Global Publishers
September 3, 2026
30 views
0 Comments

Wakili Peter Madeleka ameguswa na changamoto ya mama mjane, Asha Mbaraka anayeuguza watoto wake wawili wanaosumbuliwa na ugonjwa wa figo, taarifa zilizoibuliwa na Global TV.
Global TV iliripoti habari za mjane huyo mara kadhaa ambapo Watanzania walikuwa wakimsaidia kwa kidogo walichojaliwa ambapo leo, Madeleka ameonesha kuguswa na kumkabidhi mjane huyo kiasi cha shilingi milioni moja, fedha taslimu.

