Global Publishers
September 3, 2026
42 views
0 Comments
Jiji la Dar es Salaam la leo limebadilika kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na miaka 10 iliyopita, hususan katika sekta ya miundombinu ya barabara, ambapo miradi mbalimbali imeendelea kutekelezwa, kuboreshwa na kupanuliwa.
Baada ya kifo cha ghafla cha Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, aliyeanzisha na kusimamia miradi mbalimbali ya maendeleo nchini, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alichukua dhamana ya kuendeleza miradi hiyo pamoja na kuanzisha mingine mipya.
Hapo ndipo kauli mbiu ya “KAZI IENDELEE” ilipoendelea kushika kasi. Na leo, ukiangalia mabadiliko yanayoendelea kulipamba Jiji la Dar es Salaam, mwenye macho haambiwi tazama! 🔥🇹🇿
