Wapewa elimu mafuta, gesi asilia Tamasha la Utamaduni – HabariLeo

MOROGORO; Wananchi mbalimbali wamejitokeza kwenye banda la Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) na kupewa elimu juu ya usimamizi wa shughuli za utafutaji na uendelezaji wa mafuta na gesi asiia.

PURA ni sehemu ya taasisi mbalimbali zilizoshiriki kwenye Tamasha la Nne la Taifa la Utamaduni, Uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro na lilikuwa kivutio kikubwa kwa wananchi.

Akizungumza kwenye banda hilo, Mjiolojia kutoka PURA, Lukelo Matimbwi amewaeleza masuala mbalimbali ikiwemo tafiti zinazofanyika kuhusu masuala ya gesi asilia na pia viasharia vya uwepo wa nishati hiyo kwa baadhi ya maeneo.