Wild 4th Fruits Waleta Ladha Mpya ya Burudani Meridianbet

Global Publishers
August 24, 2026
48 views
0 Comments

Burudani ya kasino imepata ladha mpya baada ya Wild 4th Fruits kuwasili Meridianbet ukiwa na muonekano unaovutia na mfumo wa uchezaji uliotengenezwa kwa urahisi. Mchezo huu unawaleta wachezaji katika dunia iliyojaa matunda yenye rangi angavu, mazingira yenye uhai na msisimko unaojengwa kila unapocheza. Kwa wale wanaopenda michezo yenye mguso wa kisasa, Wild 4th Fruits ni moja ya chaguo jipya linaloweza kuongeza ladha kwenye burudani yako.

Kama ilivyo kwenye mchezo wowote wenye mvuto, mwanzo wa safari ndio unaochochea hamu ya kuendelea. Wild 4th Fruits imeundwa kwa mtindo unaorahisisha mchezaji kuingia moja kwa moja kwenye burudani bila kulazimika kupitia mfumo mgumu. Kila raundi inafungua ukurasa mpya, huku alama za matunda zikitoa mandhari inayokumbusha michezo ya kasino ya kizazi cha zamani.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Moja ya vitu vinavyoweza kuwavutia wachezaji ni kasi tulivu ya Wild 4th Fruits. Mchezo haujajengwa kukufanya uhisi kama unakimbizana na muda, bali unakupa nafasi ya kufurahia kila raundi na kila tukio linalotokea kwenye skrini. Hii inaufanya uwe rafiki kwa wachezaji wanaotafuta burudani rahisi baada ya siku ndefu au wanaotaka kujaribu mchezo mpya wenye mazingira mepesi.

Tayari mchezo huu umeanza kuvutia umakini kutokana na simulizi za ushindi miongoni mwa wachezaji wa Meridianbet. Kwa hiyo, Wild 4th Fruits inaweza kuwa sehemu ya burudani yako ikiwa utaicheza huku ukifurahia muonekano wake wa kipekee na safari ya kila mzunguko.

Sasa ni wakati wa kufungua mlango wa dunia yenye matunda, rangi na burudani mpya kupitia Wild 4th Fruits. Xpanse imeleta mchezo unaochanganya urahisi wa michezo na mwonekano unaoendana na kizazi cha sasa. Kama unapenda kuona kila raundi ikileta tukio jipya, mchezo huu unakualika kuuchunguza na kufurahia kila sekunde.

TAFICO waja kivingine kuimarisha sekta uvuvi – HabariLeo

DAR ES SALAAM: SHIRIKA la Uvuvi Tanzania (TAFICO), limesaini mkataba wa ujenzi wa meli mbili za uvuvi wa bahari kuu na Kampuni ya Rongcheng Xinyang Ship Industry Limited ya China, ikiwa ni hatua ya kuimarisha na kuongeza tija katika sekta ya uvuvi nchini.

Mkataba huo umesainiwa leo, Agosti 24, 2026,Jijini Dar es Salaam kupitia Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayofadhiliwa na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD).

Akizungumza wakati wa kushuhudia utiaji saini wa mkataba huo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Dk Bashiru Kakurwa, amesema hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2025 pamoja na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, kwa lengo la kuleta mapinduzi katika sekta ya uvuvi.

Dk Kakurwa ameishukuru IFAD kwa ufadhili wa ujenzi wa meli hizo kupitia AFDP, huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi katika kufungua fursa zaidi za uvuvi wa bahari kuu na kukuza uchumi wa Taifa.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Dk Jim Yonazi, amesema Ofisi ya Waziri Mkuu ikiwa Mratibu Mkuu wa AFDP, inatambua utiaji saini wa mkataba huo kuwa hatua muhimu katika utekelezaji wa programu hiyo.

Amesema ujenzi wa meli hizo ni hatua itakayochangia ukuzaji wa uchumi kupitia uvuvi wa bahari kuu, pamoja na kuongeza uwezo wa Tanzania kutumia kikamilifu rasilimali zake za bahari.

Naye Mratibu wa AFDP kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Salum Mwinjaka, amesema utiaji saini wa mkataba huo ni hatua muhimu katika kuhakikisha malengo ya programu yanafikiwa kwa wakati na utekelezaji wake unakuwa na mafanikio.

Amesema Serikali inalenga kuhakikisha walengwa wa programu pamoja na Taifa kwa ujumla wananufaika na fursa zinazotokana na utekelezaji wa AFDP.

AFDP inalenga kukuza uzalishaji endelevu wa kibiashara unaozingatia mazingira, hususan katika uzalishaji wa mbegu za mazao ya kilimo kama mahindi, alizeti, maharagwe na jamii ya mikunde, pamoja na uvuvi na ufugaji wa viumbe maji.

Programu hiyo pia inalenga kuwawezesha wanawake na kuongeza ushiriki wa vijana katika shughuli za uzalishaji.

Tume ya Jaji Lila Yaanza Kazi, Wahusika wa Ghasia za Uchaguzi Kuchunguzwa

Mwenyekiti wa Tume ya Kuchunguza Wahusika, Ghasia na Ukiukwaji wa Sheria, Jaji wa Mahakama ya Rufani, Shaban Ally Lila.

Dar es Salaam, Agosti 24, 2026 — Tume ya Kuchunguza Wahusika, Ghasia na Ukiukwaji wa Sheria Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 imeanza rasmi kazi, huku Mwenyekiti wake, Jaji wa Mahakama ya Rufani, Shaban Ally Lila, akieleza kuwa lengo kuu ni kubaini wahusika wa ghasia hizo na namna walivyoshiriki.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Jaji Lila amesema Tume hiyo imepewa jukumu la kuchunguza matukio ya ghasia, uvunjifu wa amani na madhara yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi huo.

Amesema Tume itachunguza pia chanzo cha ghasia hizo pamoja na ukiukwaji wa sheria uliojitokeza, ikiwemo kubaini watu waliohusika katika kupanga, kufadhili, kuratibu na kutekeleza matukio hayo.

Kwa mujibu wa Jaji Lila, Tume hiyo ina jukumu tofauti na Tume iliyokuwa chini ya Jaji Mstaafu Othman Chande, ambayo ilichunguza zaidi matukio ya ghasia na madhara yaliyotokea.

Tume mpya imepewa jukumu la kwenda hatua zaidi kwa kuchunguza wahusika wa ghasia hizo, namna walivyoshiriki na kiwango cha nguvu kilichotumika katika kudhibiti vurugu hizo.

Jaji Lila amesema Tume pia itachunguza madhara yaliyotokana na ghasia hizo, yakiwemo vifo, majeruhi na watu waliopotea.

Amesema Tume iliyokuwa chini ya Jaji Chande ilibainisha vifo vya watu 518, huku ikieleza kuwa huenda idadi hiyo ilikuwa kubwa zaidi kwa sababu si waathirika wote waliweza kufikiwa au kutambuliwa.

Katika utekelezaji wa majukumu yake, Tume ya Jaji Lila imepewa hadidu tano za rejea.

Hadidu ya kwanza ni kuchunguza na kubainisha wahusika wa ghasia na namna walivyoshiriki katika kupanga, kufadhili, kuratibu au kutekeleza matukio hayo.

Hadidu ya pili ni kuchunguza matukio mahsusi yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi, ikiwemo madai ya vifo visivyo vya kawaida vya watoto na watu wa makundi maalum.

Hadidu ya tatu ni kuchunguza taarifa za watu waliopotea katika maeneo yaliyokumbwa na ghasia na uvunjifu wa amani.

Hadidu ya nne ni kuchunguza madai ya matumizi ya nguvu kupita kiasi na kubaini iwapo taratibu na miongozo ya matumizi ya nguvu ilizingatiwa.

Hadidu ya tano inalipa Tume nafasi ya kuchunguza suala lolote litakaloonekana kuwa muhimu na linalohusiana na majukumu yake.

Jaji Lila amesema Tume imeundwa na Rais Samia Suluhu Hassan na kuzinduliwa rasmi Agosti 7, 2026.

Tume hiyo inaongozwa na Jaji Mstaafu Shaban Ally Lila na inajumuisha majaji wastaafu wa Mahakama Kuu, akiwemo Jaji Gad Mjemmas, Jaji Awadh Bawazir na Jaji Aishieli Sumari, pamoja na wajumbe kutoka nje ya Tanzania, akiwemo Naibu Jaji Mkuu wa Namibia na Jaji Cheborion Barishaki kutoka Uganda.

Tume ya Jaji Lila Yaanza Kazi, Wahusika wa Ghasia za Uchaguzi Wachunguzwa

Dar es Salaam, Agosti 24, 2026 — Tume ya Kuchunguza Wahusika, Ghasia na Ukiukwaji wa Sheria Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 imeanza rasmi kazi, huku Mwenyekiti wake, Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani, Shaban Ally Lila, akieleza kuwa lengo kuu ni kubaini wahusika wa ghasia hizo na namna walivyoshiriki.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Jaji Lila amesema Tume hiyo imepewa jukumu la kuchunguza matukio ya ghasia, uvunjifu wa amani na madhara yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi huo.

Amesema Tume itachunguza pia chanzo cha ghasia hizo pamoja na ukiukwaji wa sheria uliojitokeza, ikiwemo kubaini watu waliohusika katika kupanga, kufadhili, kuratibu na kutekeleza matukio hayo.

Kwa mujibu wa Jaji Lila, Tume hiyo ina jukumu tofauti na Tume iliyokuwa chini ya Jaji Mstaafu Othman Chande, ambayo ilichunguza zaidi matukio ya ghasia na madhara yaliyotokea.

Tume mpya imepewa jukumu la kwenda hatua zaidi kwa kuchunguza wahusika wa ghasia hizo, namna walivyoshiriki na kiwango cha nguvu kilichotumika katika kudhibiti vurugu hizo.

Jaji Lila amesema Tume pia itachunguza madhara yaliyotokana na ghasia hizo, yakiwemo vifo, majeruhi na watu waliopotea.

Amesema Tume iliyokuwa chini ya Jaji Chande ilibainisha vifo vya watu 518, huku ikieleza kuwa huenda idadi hiyo ilikuwa kubwa zaidi kwa sababu si waathirika wote waliweza kufikiwa au kutambuliwa.

Katika utekelezaji wa majukumu yake, Tume ya Jaji Lila imepewa hadidu tano za rejea.

Hadidu ya kwanza ni kuchunguza na kubainisha wahusika wa ghasia na namna walivyoshiriki katika kupanga, kufadhili, kuratibu au kutekeleza matukio hayo.

Hadidu ya pili ni kuchunguza matukio mahsusi yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi, ikiwemo madai ya vifo visivyo vya kawaida vya watoto na watu wa makundi maalum.

Hadidu ya tatu ni kuchunguza taarifa za watu waliopotea katika maeneo yaliyokumbwa na ghasia na uvunjifu wa amani.

Hadidu ya nne ni kuchunguza madai ya matumizi ya nguvu kupita kiasi na kubaini iwapo taratibu na miongozo ya matumizi ya nguvu ilizingatiwa.

Hadidu ya tano inalipa Tume nafasi ya kuchunguza suala lolote litakaloonekana kuwa muhimu na linalohusiana na majukumu yake.

Jaji Lila amesema Tume imeundwa na Rais Samia Suluhu Hassan na kuzinduliwa rasmi Agosti 7, 2026.

Tume hiyo inaongozwa na Jaji Mstaafu Shaban Ally Lila na inajumuisha majaji wastaafu wa Mahakama Kuu, akiwemo Jaji Gad Mjemmas, Jaji Awadh Bawazir na Jaji Aishieli Sumari, pamoja na wajumbe kutoka nje ya Tanzania, akiwemo Naibu Jaji Mkuu wa Namibia na Jaji Cheborion Barishaki kutoka Uganda.

Mchezaji Afariki Dunia Baada Ya Kuanguka Uwanjani

Global Publishers
August 24, 2026
828 views
0 Comments

Kiungo wa zamani wa West Bromwich Albion, Quévin Castro, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 25 baada ya kuanguka ghafla wakati akiichezea Real Sport Clube katika mchezo wa kirafiki nchini Ureno.

Tukio hilo lilitokea Jumamosi, Agosti 22, 2026, katika mchezo kati ya Real Sport Clube na Estrela da Amadora. Castro alianguka takribani dakika 10 baada ya mchezo kuanza na kupoteza fahamu.

Madaktari waliokuwa uwanjani walitoa huduma ya dharura na kutumia mashine ya kushtua moyo (defibrillator) kabla Castro hajapelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu zaidi.

Hata hivyo, juhudi za kumuokoa hazikufanikiwa na Castro alifariki muda mfupi baada ya kufikishwa hospitalini. Kifo chake kimetikisa soka la Ureno na Uingereza.

Castro alikuwa ameanza maisha yake ya soka nchini Uingereza na baadaye akajiunga na West Bromwich Albion mwaka 2021, ambako alicheza mechi mbili za kikosi cha kwanza. Pia aliwahi kuzichezea klabu kadhaa ikiwemo Burton Albion, Notts County, Gateshead na York City kabla ya kurejea Ureno.

Kifo hicho kimepokelewa kwa huzuni kubwa na klabu alizowahi kuzichezea, huku West Bromwich Albion ikieleza kusikitishwa na kifo cha ghafla cha mchezaji huyo mwenye umri mdogo.

Mchezo ambao Castro alianguka ulisitishwa kufuatia tukio hilo, huku jumuiya ya soka ikiendelea kutoa salamu za pole kwa familia, ndugu, marafiki na klabu yake.

Stori na Haika Urio | GPL – TUDACO

EPL na Serie A Kutamba leo, Chelsea na Roma Kuwania Pointi Tatu

Wakali wa ubashiri Tanzania, Meridianbet wanakwambia kuwa Wikendi hii ipo kwaajaili ya kuhakikisha hawakuachi patupu. ODDS KUBWA zipo kwenye mechi za leo hivyo bashiri sasa.

SERIE A kule Italia itaendelea ambapo AS Roma atakipiga dhidi ya Fiorentina ikiwa huu ni mchezo wa kuvutia sana kwani timu hizi zina historia ya kutoa mechi nzuri na ya kuvutia huku kwa ubora wa Roma ndio wanaopewa nafasi kubwa ya kuondoka na ushindi.

Timu hiyo chini ya kocha mkuu Gian Gasperini klabu hiyo ya AS Roma wanatarajiwa kuwa na msimu mzuri kwani kocha huyo anajulikana kuwa na mbinu nzuri za kunoa vikosi, huku mechi hii ikiakisi mwanzo mzuri wa ligi kwa wote. Ushindi katika mchezo wa kwanza wa ligi unaweza kutoa msingi mzuri wa kujiamini kwa kikosi katika msimu ambao Roma wanataka kupigania nafasi za juu.

Kwa upande mwingine, Fiorentina wanaingia kwenye mchezo huu wakiwa na kiu ya kubadilisha taswira yao baada ya msimu uliopita ambao haukuwa mzuri. Hata hivyo, maandalizi yao yameonyesha kwamba wana uwezo wa kuwa tishio tofauti na ilivyokuwa msimu uliopita.

Msimu uliopita, Roma liondoka na ushindi kwenye mechi zote mbili ambazo walikutana hivyo wageni wanaingia uwanjani maalumu kwaajili ya kutaka kulipa kisasi. Odds kubwa na machaguo zaidi ya 1000 yanakusubiri wewe leo. Jisajili hapa.

Piga pesa kupitia michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Lakini pia kule EPL ni Fulham dhidi ya Chelsea kutoka pale Stamford Bridge, huku mechi hii ikiwa na matarajio makubwa kwa timu zote mbili kwani ushindi pekee ndio kila timu inahitaji pale Craven Cottage.

Wenyeji wanaingia kwenye msimu huu wakiwa na mabadiliko makubwa baada ya kuahana na aliyekuwa koha wao Marco Silva baada ya kuhudumu kwa miaka mitano na kuhamia Benfica. Nafasi yake imechukuliwa na Álvaro Arbeloa, ambaye aliwahi kuwa kocha wa Real Madrid.

Chelsea nao wako kwenye mabadiliko makubwa kwani wanaanza msimu wakiwa na kocha mpya Xabi Alonso ambaye ameanza kazi kama kocha mpya baada ya klabu kumaliza msimu uliopita katika nafasi ya 10. Lengo lao kuu msimu huu ni kurudi kwenye nafasi 4 za juu yaani Top Four.

The Blues wamefanya mabadiliko makubwa kwenye kikosi, huku wakisajili wachezaji kama Morgan Rogers kwa £117m, Lacroix, na wachezaji wenye uzoefu mkubwa kama vile Jordan Henderson na Danny Welbeck.

Kwenye maandalizi ya mwisho ya msimu, Chelsea waliifunga Real Sociedad 3-1, jambo linalompa Alonso matumaini kabla ya mchezo huu wa ligi ambao unatarajiwa kuwa mgumu ugenini.

Fulham wanapata faida ya kutumia uwanja wa nyumbani kwani kutakuwa na mashabiki zao lakini hiyo haiwafanyi The Blues washindwe kufanya vizuri, kwani timu ambayo imejipanga vyema ndio inaweza kuondoka na ushindi. Beti sasa.

Quevin Castro Afariki Dunia Baada Ya Kuanguka Uwanjani

Global Publishers
August 24, 2026
36 views
0 Comments

Kiungo wa zamani wa West Bromwich Albion, Quévin Castro, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 25 baada ya kuanguka ghafla wakati akiichezea Real Sport Clube katika mchezo wa kirafiki nchini Ureno.

Tukio hilo lilitokea Jumamosi, Agosti 22, 2026, katika mchezo kati ya Real Sport Clube na Estrela da Amadora. Castro alianguka takribani dakika 10 baada ya mchezo kuanza na kupoteza fahamu.

Madaktari waliokuwa uwanjani walitoa huduma ya dharura na kutumia mashine ya kushtua moyo (defibrillator) kabla Castro hajapelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu zaidi.

Hata hivyo, juhudi za kumuokoa hazikufanikiwa na Castro alifariki muda mfupi baada ya kufikishwa hospitalini. Kifo chake kimetikisa soka la Ureno na Uingereza.

Castro alikuwa ameanza maisha yake ya soka nchini Uingereza na baadaye akajiunga na West Bromwich Albion mwaka 2021, ambako alicheza mechi mbili za kikosi cha kwanza. Pia aliwahi kuzichezea klabu kadhaa ikiwemo Burton Albion, Notts County, Gateshead na York City kabla ya kurejea Ureno.

Kifo hicho kimepokelewa kwa huzuni kubwa na klabu alizowahi kuzichezea, huku West Bromwich Albion ikieleza kusikitishwa na kifo cha ghafla cha mchezaji huyo mwenye umri mdogo.

Mchezo ambao Castro alianguka ulisitishwa kufuatia tukio hilo, huku jumuiya ya soka ikiendelea kutoa salamu za pole kwa familia, ndugu, marafiki na klabu yake.

Stori na Haika Urio | GPL – TUDACO

Aishi na Uvimbe Miaka 20 Aomba Msaada wa Matibabu, Afunguka Mazito -Video

Global Publishers
August 24, 2026
90 views
0 Comments

Usemi wa Kiswahili “Kabla hujafa hujaumbika” unaakisi kwa kiasi kikubwa maisha ya Ester Juma, mwenye umri wa miaka 32, mkazi wa Tabata Barakuda jijini Dar es Salaam, ambaye kwa zaidi ya miaka 20 amekuwa akiishi na uvimbe mkubwa usoni.

Ester anapitia wakati mgumu huku akihangaika kutafuta fedha kwa ajili ya matibabu na upasuaji wa kuondoa uvimbe huo ambao umeathiri kwa kiasi kikubwa maisha yake ya kila siku.

Akizungumza kuhusu hali yake, Ester amesema amekuwa akikumbana na changamoto mbalimbali anapokuwa katika maeneo ya umma. Anaeleza kuwa baadhi ya watoto humkimbia wanapomuona, huku wakati mwingine hata mtoto wake mwenyewe akimuogopa kutokana na mabadiliko ya sura yake.

Changamoto hiyo, amesema, imemfanya kuishi maisha yenye maumivu na msongo mkubwa huku akiwa na matumaini ya kupata msaada wa matibabu.

Ester amesema aliwahi kufika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kupata matibabu, lakini hakufanikiwa kuanza mchakato huo baada ya kushindwa kupata Shilingi 450,000 zinazohitajika kwa ajili ya vipimo.

Kwa sasa, Ester anaendelea kuomba msaada kutoka kwa wasamaria wema ili aweze kupata fedha za vipimo na hatimaye kufanyiwa upasuaji.

Mtu yeyote aliyeguswa na hali ya Ester na angependa kumsaidia anaweza kuchangia kupitia namba 0760 780914, jina Magoli Juma.

Brighton Yaichakaza Aston Villa 4-0, Liverpool Yaokolewa Na Penalti Ya Dakika Za Mwisho

Brighton imeanza kwa kishindo msimu wa 2026/27 wa Ligi Kuu England baada ya kuichapa Aston Villa mabao 4-0 katika mchezo uliochezwa Jumapili, Agosti 23, 2026, kwenye Uwanja wa Amex.

Brighton ilianza mchezo kwa kasi na kupata bao la kuongoza dakika ya nane baada ya Victor Lindelöf kujifunga mwenyewe.

Dakika 10 baadaye, Maxim De Cuyper aliongeza bao la pili na kuifanya Brighton kuendelea kutawala mchezo.

Jack Hinshelwood aliendelea kuiumiza Aston Villa baada ya kufunga mabao mawili ndani ya dakika mbili, akitikisa nyavu dakika ya 30 na 31 na kuifanya Brighton kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 4-0.

Hali ilizidi kuwa ngumu kwa Aston Villa dakika ya 40 baada ya João Gomes kuonyeshwa kadi nyekundu kufuatia kumchezea vibaya mchezaji wa Brighton.

Villa hivyo ilimaliza kipindi cha kwanza ikiwa pungufu kwa mchezaji mmoja, huku Brighton ikiwa tayari imeweka msingi wa ushindi mkubwa.

LIVERPOOL YAOKOLEWA DAKIKA ZA MWISHO

Katika mchezo mwingine wa Ligi Kuu England, Liverpool imelazimishwa sare ya mabao 2-2 na Newcastle United kwenye Uwanja wa St James’ Park.

Newcastle ilianza kwa kasi na kupata bao la kuongoza dakika ya tano kupitia Anthony Elanga.

Liverpool ilirejea kipindi cha pili na kusawazisha kupitia Cody Gakpo dakika ya 55, kabla ya Joe Willock kuirudisha Newcastle kifua mbele dakika mbili baadaye.

Liverpool iliendelea kusaka bao la kusawazisha hadi dakika za mwisho, ambapo ilipata penalti katika muda wa nyongeza.

Dominik Szoboszlai alitulia na kufunga mkwaju huo dakika ya 90+9, akiipa Liverpool pointi moja katika mchezo wake wa kwanza wa msimu.

Matokeo hayo yameifanya Liverpool kuanza kampeni ya msimu wa 2026/27 kwa sare, huku kocha mpya Andoni Iraola akianza rasmi safari yake katika Ligi Kuu England.

Stori na Haika Urio | GPL – TUDACO

Binti wa Museveni Atawazwa Kuwa Askofu wa Kanisa la CNC Uganda

KAMPALA, Uganda — Pastor Patience Rwabwogo, binti wa Rais wa Uganda Yoweri Museveni, ametawazwa kuwa Askofu wa Covenant Nations Church (CNC) katika ibada iliyofanyika Jumapili, Agosti 23, 2026.

Hafla hiyo ilifanyika katika kampasi ya CNC Maya, Kyengera Town Council, Wilaya ya Wakiso, na kuhudhuriwa na Rais Museveni pamoja na Mama Janet Museveni, wazazi wa Patience na viongozi wa Uganda.

Miongoni mwa viongozi wengine waliohudhuria ni Makamu wa Rais Jessica Alupo, Makamu Mwenyekiti wa Taifa wa NRM Moses Kigongo, mawaziri, viongozi wa vyombo vya usalama akiwemo Inspekta Jenerali wa Polisi Abbas Byakagaba, wanadiplomasia na viongozi mbalimbali wa dini.

Ibada hiyo ilifikia kilele muda mfupi baada ya saa 8:00 mchana, ambapo Askofu maarufu kutoka Marekani, Dk. LaDonna Osborn, alimwita Pastor Patience mbele kwa ajili ya kutawazwa rasmi kuwa Askofu.

Katika mahubiri yake akitumia vifungu vya Luka 4:8-21, Osborn alimtaka Askofu Patience kukubali kikamilifu jukumu la kuhubiri Kristo, kulijenga Kanisa na kuendeleza ufalme wa Mungu.

Kabla ya utawazo huo, wazee wa CNC wakiongozwa na Allen Kagina walitoa uthibitisho wa wito na uwezo wa Patience kuongoza kama Askofu.

Walisema Patience ndiye mwanzilishi na mchungaji mkuu wa CNC, wakieleza kuwa kanisa hilo lilianza takribani miaka 20 iliyopita kama kikundi kidogo cha waumini kilichokuwa kikikutana nyumbani.

Kwa mujibu wa wazee hao, huduma hiyo imekua kupitia maombi, uvumilivu na mafanikio ya kiroho na sasa imejikita katika mafundisho ya Biblia, uanafunzi, maombi, ibada, uongozi, uinjilisti na huduma kwa jamii.

Viongozi hao pia wamepongeza mchango wa Patience kwa vijana, wakiwemo wanafunzi na wataalamu vijana, kupitia mafundisho ya Biblia, ushauri, mikutano ya uongozi na shughuli za uinjilisti.

Wamesema huduma yake imewahamasisha waumini kutumia elimu, vipaji na fursa walizonazo kwa ajili ya utukufu wa Mungu na manufaa ya jamii.

Kutawazwa kwake kuwa Askofu kunatajwa kuwa hatua muhimu katika safari yake ya zaidi ya miongo miwili ya huduma ya kidini.

Stori na Na Ashura Karimu | GPL -TUDACO