Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Michezo

Miaka 11 Baada Ya Kustaafu, Ronaldinho Arejea Kwenye Soka

By admin
August 22, 2026 2 Min Read
Comments Off on Miaka 11 Baada Ya Kustaafu, Ronaldinho Arejea Kwenye Soka

Milan, Italia — Mwanasoka nguli wa Brazil, Ronaldinho Gaúcho, anatarajiwa kurejea rasmi uwanjani akiwa na umri wa miaka 46, miaka 11 baada ya kucheza mchezo wake wa mwisho wa soka la ushindani.

Ronaldinho amefikia makubaliano na Ravenna FC, klabu ya Italia inayoshiriki Serie C, ambapo atahusishwa na klabu hiyo si tu kama mwekezaji, bali pia kama mchezaji.

Mpango huo unalenga kumrudisha nyota huyo wa zamani uwanjani kwa mara nyingine, huku akipewa nafasi ya kuandika ukurasa wa mwisho wa safari yake ya soka kwa kujaribu kufunga bao akiwa amevalia jezi ya Ravenna.

Hata hivyo, hadi sasa tarehe rasmi ya mchezo ambao Ronaldinho atarejea uwanjani haijatangazwa.

Ronaldinho, ambaye alistaafu soka baada ya kucheza mchezo wake wa mwisho akiwa na Fluminense mwaka 2015, sasa anarejea katika kipindi ambacho Ravenna inashiriki Serie C, daraja la tatu la soka nchini Italia.

Klabu hiyo pia inalenga kutumia jina na umaarufu wa Ronaldinho kuongeza mvuto wake kimataifa na kusaidia katika mpango wake wa kujenga upya timu.

Ronaldinho ni miongoni mwa wanasoka walioacha alama kubwa katika historia ya mchezo huo. Akiwa na Barcelona, alitwaa Ballon d’Or mwaka 2005 na kusaidia klabu hiyo kushinda UEFA Champions League mwaka 2006.

Pia alikuwa sehemu ya kikosi cha Brazil kilichotwaa Kombe la Dunia mwaka 2002, akicheza pamoja na nyota wengine wakubwa wa kizazi chake.

Iwapo atashuka uwanjani kama ilivyopangwa, kurejea kwa Ronaldinho akiwa na miaka 46 kutakuwa tukio la kipekee kwa mashabiki wa soka duniani, hasa wale waliovutiwa na kipaji chake cha kipekee wakati wa enzi zake.

STORI NA RAZAKU RAMADHAN, GPL – TUDACO

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Siri Nzito! Ndege Ya Malaysia Iliyopotea Angani, Haijulikani Ilipoelekea-Video

Next

Roboti Yaanguka Kwa Hitilafu ya Umeme Wakati wa Mazoezi

Recent Posts

  • Mavunde Ampongeza Ndejembi “Ni Kiongozi Kijana, Mwadilifu na Mzalendo” – Video
  • MWABUKUSI: KUFUKUZWA CCM KWA NCHIMBI HAKUMVUI MOJA KWA MOJA UMAKAMU WA RAIS
  • Dili la Sh Bilioni 418! Liverpool Yafikia Makubaliano na PSG kwa Barcola
  • Droo ya UEFA Champions League Msimu wa 2026/27 Kufanyika Leo Monaco
  • Kesi ya Uhaini ya Lissu Yaendelea leo;- Maswali Mazito Yaibuka Katika Dodoso la Serikali

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme