Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Subscribe
Close

Search

Habari

Wakurugenzi wa Halmashauri wabebeshwa zigo la mazingira

By admin
August 17, 2026 2 Min Read
0

Dodoma. Wakurugenzi wa halmashauri nchini Tanzania wameagizwa kusimamia na kuwa mfano wa kupunguza matumizi ya plastiki katika ofisi zao ili kulinda mazingira.

Agizo hilo limetolewa leo Januari 17, 2026 na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Profesa Peter Msofe wakati akizindua mradi wa urejeshaji wa mazingira na uoto wa asili.

Mradi huo wa miaka mitano unasimamia na World Wildlife Fund (WWF) na kutekelezwa katika Wilaya za Mpwapwa na Chamwino (Dodoma) na Korogwe na Kilindi (Tanga).


Profesa Msofe amesema ni aibu wakurugenzi kuwa waangalizi kwenye uharibifu wa mazingira na hawatakiwi kuwa wapanga kazi badala yake wawe wasimamizi wa kazi hizo wakianzia wao kuonyesha mfano.

“Katika hili sitaki mkafanye, bali naagiza lazima litekelezwe tena iwe nchini nzima, na mshirikishe walio chini yenu na jamii inayowazunguka, lazima mtambue kwenye mazingira tuna hali mbaya na hivyo hatuwezi kucheka,” amesema Profesa Msofe.

Kuhusu mradi huo amesema ni lazima uwe wa kiushindani katika mpango wa urejeshaji wa uoto wa asili ambapo Tanzania imejenga kufikia hekta milioni 5.2 wakati bara la Afrika ni hekta milioni 100 na kwa upande wa Dunia zinatakiwa kufikia hekta milioni 350 ifikapo 2050.

Ofisa kutoka WWF Almas Kashindye ametaja lengo katika mradi huo ni kuboresha maisha ya wananchi na kulinda bayonuwai.

Kashindye amesema mradi huo unagharimu Sh5.4 bilioni huku walengwa zaidi wakiwa watu wa vijijini katika wilaya zilizoonekana kuwa na uharibifu mkubwa wa mazingira.

Msimamizi wa mradi huo uliopewa jina la IKI Forest Landscape, Raymond Kallenga amesema mbali na Tanzania mpango huo unatekelezwa kwa nchi za Uganda, Madagasca, Brazil, Peru na Colombia na mfadhiri ni Ujerumani.

Killenga anasema mkakati waliouweka ni ufuatiliaji zaidi katika kila hatua ili kuhakikisha wanapata matokeo kama ilivyo.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Wadau wataka mipango ya tabianchi izingatie jinsia

Next

MUHAS yaanzisha tiba ya kibingwa ya kinywa, meno kwa watoto

No Comment! Be the first one.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recent Posts

  • VETA YAANDAA MTAALA WA MAFUNZO YA MUDA MFUPI WA FANI YA RECYCLING
  • VETA IMETAKIWA KUENDELEA KUWASHIRIKISHA WATAALAMU WALIOBOBEA FANI MBALIMBALI
  • BAHI IMETENGA MILLION 100 KUTOKA MAPATO YAKE YA NDANI KUSAIDIA VIJANA WA WILAYA KUPATA ELIMU VETA
  • *WAKULIMA WA KITOMONDO WANUFAIKA NA HUDUMA YA MAWASILIANO*
  • MAGAZETINI LEO JUMATATU AGOSTI 17/2026

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme