Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

TRA Songwe kuanzisha klabu za kodi shule za sekondari

By admin
August 17, 2026 2 Min Read
0

Songwe. Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Songwe imeanza mchakato wa kuanzisha klabu za kodi katika shule zote za sekondari mkoani humo, ikiwa ni mkakati wa kuwajengea wanafunzi uelewa kuhusu umuhimu wa kulipa kodi.

Klabu hizo zinalenga pia kuwawezesha wanafunzi kufahamu masuala ya kodi na kuyafikisha katika jamii, hususan umuhimu wa kudai na kutoa risiti wakati wa manunuzi na kufanya biashara.

Kaimu Meneja wa TRA Mkoa wa Songwe, Angetile Kitalile, amesema hayo leo Jumatatu, Agosti 17, 2026, wakati wa uzinduzi wa klabu ya kodi katika Shule ya Sekondari Mlowo wilayani Mbozi.



Amesema hadi sasa mamlaka hiyo imefanikiwa kuanzisha klabu saba katika shule za sekondari mkoani humo na mpango ni kuzifikia shule zote katika halmashauri za mkoa huo.

“Mpaka sasa tumefanikiwa kufungua klabu saba za kodi katika shule za sekondari. Leo tumeifikia Shule ya Sekondari Mlowo iliyopo hapa Wilaya ya Mbozi, ikiwa ni mwendelezo wa mpango huu, tukiamini wanafunzi watasaidia kuifikisha elimu hiyo katika jamii wanayoishi,” amesema.

Kitalile amesema klabu hizo ni miongoni mwa njia zinazotumiwa na TRA kutoa elimu kwa walipa kodi wa sasa na kuwaandaa walipa kodi wa baadaye.

Amesema wanafunzi watakaopata elimu hiyo wataweza kuelewa wajibu wa kila mwananchi katika kulipa kodi na umuhimu wa kudai risiti wanaponunua bidhaa au kupata huduma.

Kwa mujibu wa Kitalile, elimu hiyo pia itasaidia kujenga utamaduni wa kufuata taratibu za kodi na kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu mchango wa kodi katika maendeleo ya Taifa.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Mlowo, Sophia Luoga, amepongeza hatua hiyo akisema itawajengea wanafunzi uzalendo na kuwafanya kuwa mabalozi wazuri wa masuala ya kodi katika familia na jamii.

Amesema matarajio yao ni kuona elimu inayotolewa kupitia klabu hizo ikisaidia kizazi cha sasa na kijacho kuelewa wajibu wa kulipa kodi wakati wa kununua au kuuza bidhaa.

“Wanafunzi wataelewa kuwa kila Mtanzania ana wajibu wa kulipa kodi na kwamba wakati wa kununua bidhaa au kufanya biashara, ni muhimu kutoa na kudai risiti ili Taifa lipate mapato ya kuendeleza miradi ya maendeleo,” amesema.

Baadhi ya wanafunzi walioshiriki kuanzishwa kwa klabu hiyo wamesema mpango huo utawasaidia kupata uelewa zaidi kuhusu masuala ya kodi, ikiwamo umuhimu wa kudai na kutoa risiti sahihi wanaponunua bidhaa au kufanya biashara.

Wamesema watatumia elimu watakayoipata kuwafikishia wazazi, ndugu na wananchi wengine ili kuongeza uelewa kuhusu ulipaji kodi na mchango wake katika maendeleo ya Taifa.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

GLOBAL EDUCATION LINK YAPELEKA WANAFUNZI 198 CHINA NA 189 INDIA

Next

Agizo la Chalamila Stendi ya Magufuli lapingwa

No Comment! Be the first one.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recent Posts

  • Serikali yatoa siku nane kwa wazalishaji saruji kushusha bei
  • Mchengerwa ataja vipaumbele sita kupunguza vifo vya mama, mtoto
  • Babu adai kupigwa ngwara na mwalimu Bahi
  • Kibwagizo cha wimbo wa ‘kilio cha mtu mzima’ kilivyotumika kesi ya ardhi
  • Mwili wa mtoto wa miaka saba wakutwa shimoni Tabora

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme