Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Burudani

Rais Samia Ateua na Kuhamisha Wakuu Wa Mikoa, Makatibu Tawala

By admin
August 27, 2026 2 Min Read
Comments Off on Rais Samia Ateua na Kuhamisha Wakuu Wa Mikoa, Makatibu Tawala

Global Publishers
August 27, 2026
54 views
0 Comments

Dar es Salaam, Agosti 27, 2026 — Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi na uhamisho wa Wakuu wa Mikoa pamoja na Makatibu Tawala wa Mikoa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari S. Machumu, uteuzi na uhamisho huo umefanyika kama ifuatavyo:

UTEUZI WA WAKUU WA MIKOA
  1. CP. Salum Rashid Hamduni, aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.
  2. Alexander Pastory Mnyeti ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita.
  3. Stanslaus Haroon Nyongo ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
  4. Jumanne Abdallah Sagini ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.
UHAMISHO WA WAKUU WA MIKOA
  1. Martine Reuben Shigela amehamishwa kutoka Mkoa wa Geita kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara.
  2. Said Mohamed Mtanda amehamishwa kutoka Mkoa wa Mwanza kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, akichukua nafasi ya Anamringu Macha ambaye amestaafu.
  3. Abubakar Mussa Kunenge amehamishwa kutoka Mkoa wa Pwani kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe, akichukua nafasi ya Jabiri Omari Makame, ambaye atapangiwa majukumu mengine.
  4. Beno Moris Malisa amehamishwa kutoka Mkoa wa Mbeya kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora. Anachukua nafasi ya Paul Matiko Chacha, ambaye aliteuliwa kuwa Katibu wa NEC – Idara ya Oganaizesheni ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
  5. Adam Kighoma Malima amehamishwa kutoka Mkoa wa Morogoro kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Lindi, akichukua nafasi ya Zainab Telack, ambaye amestaafu.
  6. Queen Cuthbert Sendiga amehamishwa kutoka Mkoa wa Manyara kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.
UTEUZI NA UHAMISHO WA MAKATIBU TAWALA WA MIKOA

Uteuzi

Richard Marcellino Kayombo ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani.

Uhamisho

  1. Bw. Balandya Mayuganya Elikana amehamishwa kutoka Mkoa wa Mwanza kwenda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya.
  2. Dkt. Fatuma Ramadhan Mganga amehamishwa kutoka Mkoa wa Singida kwenda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza.
  3. Pili Hassan Mnyema amehamishwa kutoka Mkoa wa Pwani kwenda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga.
  4. Rodricks Lazaro Mpogolo amehamishwa kutoka Mkoa wa Mbeya kwenda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa upashaji wa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa wateule utafanyika kwa tarehe itakayopangwa baadaye.

Uteuzi na uhamisho huo umetangazwa na Ikulu, Dar es Salaam, Agosti 27, 2026.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI NA UHAMISHO WA WAKUU WA MIKOA

Recent Posts

  • Rais Samia Ateua na Kuhamisha Wakuu Wa Mikoa, Makatibu Tawala
  • RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI NA UHAMISHO WA WAKUU WA MIKOA
  • Mavunde Ampongeza Ndejembi “Ni Kiongozi Kijana, Mwadilifu na Mzalendo” – Video
  • MWABUKUSI: KUFUKUZWA CCM KWA NCHIMBI HAKUMVUI MOJA KWA MOJA UMAKAMU WA RAIS
  • Dili la Sh Bilioni 418! Liverpool Yafikia Makubaliano na PSG kwa Barcola

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme