Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Asimulia alivyojifungua katikati ya tetemeko la ardhi

By admin
August 17, 2026 2 Min Read
0

Dar es Salaam. Maria Florida, 39, ameeleza furaha yake baada ya kujifungua salama mtoto wake wa nne kwa njia ya upasuaji, huku tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 7.7 likitikisa eneo la Nusa Tenggara Mashariki mwa Indonesia.

Florida alikuwa tayari ameshaanza kufanyiwa upasuaji katika Hospitali ya Nagekeo wakati tetemeko hilo lilipoanza. Hata hivyo, madaktari waliendelea na huduma huo licha ya mazingira magumu yaliyosababishwa na mtikisiko huo.

Tetemeko hilo lilisababisha kukatika kwa umeme hospitalini hapo, hivyo madaktari walilazimika kutumia mwanga wa tochi kuendelea na upasuaji hadi kufanikisha kumleta duniani mtoto huyo.



Baada ya kujifungua mtoto wa kike, Florida alimpa jina Gempita Soli Wona,   linalohusishwa na neno la Kiindonesia linalomaanisha tetemeko la ardhi.

Mtoto huyo alizaliwa akiwa na uzito wa kilo 1.3 na kwa mujibu wa taarifa za madaktari afya yake inaendelea kuimarika.

Tetemeko hilo lilitokea Agosti 15, 2026 na kuleta madhara makubwa mashariki mwa Indonesia, likisababisha vifo vya watu wasiopungua 54, majeruhi zaidi ya 130 na kuwalazimisha maelfu ya wakazi kuondoka katika maeneo yaliyoathirika.

Kutokana na mitikisiko kuendelea na baadhi ya miundombinu ya hospitali kuathirika, mtoto huyo amewekwa katika mashine maalumu ya kuhifadhi joto iliyowekwa nje ya jengo la hospitali.

Florida amewashukuru madaktari kwa kujitoa na kuendelea na upasuaji huo licha ya hatari iliyokuwapo.

Wakati tukio hilo likitoa simulizi ya matumaini, idadi ya watu waliofariki kutokana na tetemeko hilo imefikia 53, huku shughuli za uokoaji zikiendelea katika maeneo yaliyoathirika.

Waokoaji wamefanikiwa kupata miili mingine sita, hali iliyoongeza idadi ya vifo kutoka 47 hadi 53.

Zaidi ya watu 135 wameripotiwa kujeruhiwa, huku nyumba zaidi ya 900 zikiharibiwa na maelfu ya watu kulazimika kuondoka katika makazi yao kutokana na hofu ya mitetemeko zaidi.

Takriban watu 5,000 wamehama makazi yao na kuhamia maeneo salama likiwa la  Kisiwa cha Flores.

Tetemeko hilo pia limesababisha maporomoko ya ardhi na kuziba baadhi ya barabara, hali iliyowapa changamoto waokoaji kuwafikia watu waliokwama katika maeneo yaliyoathirika zaidi.

Kukatika kwa umeme na mawasiliano kumeongeza ugumu wa shughuli za uokoaji, huku mamlaka zikiendelea kuratibu juhudi za kuwafikia waathirika na kutoa msaada wa dharura.

Misaada inayotolewa inajumuisha chakula, mahema na mahitaji mengine muhimu kwa watu walioathirika.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Jose Chameleone alivyoibua shangwe akitumbuiza kilele tamasha la Kizimkazi

Next

Kwa nini GB 128 za simu yako zinawahi kujaa? Fanya hivi…

No Comment! Be the first one.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recent Posts

  • Wafugaji walalamikia operesheni za usiku, Serikali yajibu
  • Tanzania, DR Congo kuimarisha ushirikiano, kuondoa vikwazo
  • Watano wafariki dunia akiwamo mtoto mchanga, wanane wajeruhiwa Lushoto
  • Madeleka aeleza namna alivyokamatwa Mahakama Kuu
  • Makosa matatu yasababisha daladala 203 kufungiwa VTS

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme