Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Mradi wa maji wa miji 28 Geita wafikia 80% – HabariLeo

By admin
August 26, 2026 2 Min Read
Comments Off on Mradi wa maji wa miji 28 Geita wafikia 80% – HabariLeo

GEITA: MRADI mkubwa wa maji wa miji 28 unaotekelezwa kwa gharama ya Dola za Marekani Milioni 53.463 ndani ya Manispaa ya Geita umefikia asilimia 80 ya utekelezaji.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Geita (GEUWASA) Mhandisi Frank Changawa ametoa taarifa hiyo kwa viongozi wa mbio za Mwenge mwaka 2026 walipotembelea kituo cha kusukuma maji.

Mhandisi Changawa alisema mkandarasi wa mradi huo tayari amelipwa Dola za Kimarekani Milioni 37.47 ambapo mradi umesanifiwa kuhudumia wakazi zaidi ya 700,000 kwa asilimia 100 katika ata zote 13 za Manispaa ya Geita.

Amesema mkataba wa mradi huo wa Maji wa Miji 28 ulisaniwa mwezi Juni 2022 huku utekelezaji wa mradi ukianza rasmi Aprili 11 na awali ulipangwa kutekelezwa kwa miezi 32 na kukamilika ifikapo Disemba 2025.

Mhandisi Changawa amesema kutokana na changamoto za upatikanaji wa eneo la kujenga chanzo cha maji, mradi umeongezewa muda wa utekelezaji na sasa unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 30 Septemba 2026.

“Ujenzi wa chanzo chenye ukubwa wa lita milioni 46 kwa siku kwenye ziwa Viktoria katika eneo la Senga umefikia asilimia 80 huku Ujenzi wa Kituo cha kusukuma Maji chenye ukubwa wa lita milioni tatu umefikia asilimia 85.

“Ujenzi wa chujio lenye ukubwa wa lita milioni 45 kwa siku umefikia asilimia 75 huku ujenzi wa Matenki matano ya kuhifadhia maji umefikia wastani wa asilimia 95”, amesema.

Mhandisi Changawa ameongeza kuwa kazi ya ulazaji wa bomba kuu lenye kipenyo cha 150mm hadi 800mm urefu wa km 76.47 kutoka kwenye chujio hadi kwenye matanki matano ya kuhifadhia maji umefikia asilimia 95

“Aidha uazaji wa mabomba ya usambazaji wa maji yenye kipenyo cha milimita 75 hadi 400 urefu wa kilometa 30 umefikia asilimia 10”, amesema Mhandisi Changawa.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2026, Wazo Michael Mwang’oda amesifu maendeleo ya mradi na huo na kuwaomba wananchi kulinda miundombinu ya mradi ili kusaidia kufikiwa lengo la serikali kupunguza changamoto ya maji.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Aishi na Uvimbe Miaka 20 Aomba Msaada wa Matibabu, Afunguka Mazito -Video

Next

MWANAMUZIKI DOLLY PARTON AFARIKI AKIWA NA MIAKA 80

Recent Posts

  • Rais Samia Ateua na Kuhamisha Wakuu Wa Mikoa, Makatibu Tawala
  • RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI NA UHAMISHO WA WAKUU WA MIKOA
  • Mavunde Ampongeza Ndejembi “Ni Kiongozi Kijana, Mwadilifu na Mzalendo” – Video
  • MWABUKUSI: KUFUKUZWA CCM KWA NCHIMBI HAKUMVUI MOJA KWA MOJA UMAKAMU WA RAIS
  • Dili la Sh Bilioni 418! Liverpool Yafikia Makubaliano na PSG kwa Barcola

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme