Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Mtoto wa Kim Kardashian na Kanye West Afunguka Mazito ‘Ataja Kampuni ya Kahawa’

By admin
August 26, 2026 2 Min Read
Comments Off on Mtoto wa Kim Kardashian na Kanye West Afunguka Mazito ‘Ataja Kampuni ya Kahawa’

Mtoto wa mastaa Kim Kardashian na Kanye West, North West,  amesema anatamani kuwa na maisha ya kawaida na kupata kazi ya kawaida, licha ya kuwa tayari ameanza kujijengea jina katika ulimwengu wa burudani akiwa na umri mdogo.

North, ambaye kwa sasa ana miaka 13, amefichua kuwa anatamani kufanya kazi katika katika kampuni ya kuuza kahawa mwaka ujao, akisema anataka kupata uzoefu wa kuwa na “kazi ya kawaida” kama watu wengine.

Akizungumza katika mahojiano yake na jarida la Dazed, North alisema bado ana hamu ya kufanya kazi na kwamba moja ya ndoto zake ni kuwa mhudumu wa kahawa.

“Bado nataka kufanya kazi. Nataka kufanya kazi Starbucks mwaka ujao. Nafikiri naweza kwa sababu nitakuwa na miaka 14. Nataka kuwa na kazi ya kawaida, nadhani,” alisema North.

Kauli hiyo imekuja licha ya North tayari kuanza safari yake katika ulimwengu wa umaarufu. Amejishughulisha na muziki, amewahi kushiriki katika maonesho ya jukwaani na pia kuonekana katika maudhui mbalimbali ya mitindo.

Kutokana na wazazi wake kuwa miongoni mwa watu maarufu duniani, North amekuwa akifuatiliwa na vyombo vya habari tangu akiwa mtoto.

Hata hivyo, sasa anaonekana kutamani kupata uzoefu tofauti na maisha ya umaarufu, akitaka kujua namna watu wengine wanavyoishi na kufanya kazi za kawaida.

Katika mahojiano hayo, North pia alizungumzia mwonekano wake, ikiwemo nywele zake za bluu na ambazo zimekuwa zikizungumziwa mitandaoni.

Akijibu wanaokosoa mwonekano huo, alisema watu wengi wanafanya mambo mengine anayoyaona kuwa mabaya, huku yeye akisisitiza kuwa anachotaka ni kuwa na nywele za bluu.

Licha ya kuwa bado ni kijana, North tayari ameanza kujenga utambulisho wake nje ya umaarufu wa wazazi wake, huku kauli yake kuhusu kutaka kufanya kazi Starbucks ikionyesha namna anavyotamani kupata maisha yenye uzoefu wa kawaida.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

MAGAZETINI LEO JUMATANO AGOSTI 26/2026

Next

Marekani Yawasaka Makamanda Wa IRGC, Yaweka Zawadi Ya Bilioni 26.5 – Video

Recent Posts

  • Rais Samia Ateua na Kuhamisha Wakuu Wa Mikoa, Makatibu Tawala
  • RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI NA UHAMISHO WA WAKUU WA MIKOA
  • Mavunde Ampongeza Ndejembi “Ni Kiongozi Kijana, Mwadilifu na Mzalendo” – Video
  • MWABUKUSI: KUFUKUZWA CCM KWA NCHIMBI HAKUMVUI MOJA KWA MOJA UMAKAMU WA RAIS
  • Dili la Sh Bilioni 418! Liverpool Yafikia Makubaliano na PSG kwa Barcola

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme