Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Kwa nini shahada yako si tiketi tena ya ajira

By admin
August 18, 2026 3 Min Read
Comments Off on Kwa nini shahada yako si tiketi tena ya ajira

Dar es Salaam. Wakati maelfu ya vijana wa Tanzania wakijiandaa kuhitimu kutoka vyuo vikuu na taasisi za elimujuu mwaka huu, wataalamu wa elimu na wadau wa maendeleo ya vijana,  wameonya kuwa kuwa na shahada pekee hakutoshi tena kupata ajira katika soko la ajira linalozidi kuwa na ushindani mkubwa na kuendeshwa na maendeleo ya teknolojia.



Onyo hilo linakuja wakati wahitimu wengi wanaingia kwenye soko la ajira wakiwa na matarajio yasiyoendana na uhalisia wa fursa zilizopo, huku wengine wanaojaribu kujipatia kipato kupitia biashara za mtandaoni na kazi za kujitegemea, wakikumbana na changamoto ya kujenga utambulisho imara wa kitaaluma.

Akizungumza katika mkutano wa mradi uitwao Career Development Project Summit 2026, ulioandaliwa na Save Youths Dreams Foundation hivi karibuni jijini Dar es Salaam, Meneja wa mradi huo, Winny Kaaya, alisema kuna umuhimu mkubwa wa kuwapa wanafunzi nafasi ya kukutana na waajiri, wajasiriamali na wataalamu kabla ya kuhitimu masomo yao.

Alisema vijana wengi huhitimu vyuo vikuu wakiwa na uelewa mdogo kuhusu matarajio ya waajiri, umuhimu wa kujenga mitandao ya kitaaluma pamoja na fursa zilizopo nje ya ajira rasmi.

“Lengo la mkutano huu ni kuwapa wanafunzi na wahitimu maarifa ya vitendo kuhusu uwezo wa kuajirika, kujenga utambulisho wa kitaaluma na kutambua fursa zilizopo katika ujasiriamali, uchumi wa kidijitali na sekta binafsi,” alisema.

Kaaya aliongeza kuwa aina hiyo ya mafunzo huwasaidia vijana kufanya uamuzi sahihi kuhusu taaluma zao na kujenga mitandao itakayowawezesha kupata fursa hata baada ya kuhitimu.

Katika mkutano huo, umuhimu wa kujenga sifa njema na kuzingatia maadili binafsi pia vilisisitizwa. Kiongozi wa Mahusiano ya Umma na Mawasiliano ya Kimkakati wa taasisi ya Empower, Furahini Godlike, aliwataka vijana kuzingatia uadilifu, uwajibikaji na uaminifu kama nguzo muhimu za mafanikio katika taaluma zao.

Alisema waajiri na washirika wa biashara hawazingatii vyeti vya kitaaluma pekee, bali pia huangalia kiwango cha uaminifu, nidhamu na maadili ya mtu.

“Maadili yako yanaongoza uamuzi wako, na uamuzi wako ndiyo unaoamua jinsi watu watakavyokukumbuka,” alisema.

Majadiliano hayo pia yaligusia mustakabali wa ajira, ambapo maendeleo ya teknolojia yanaendelea kubadilisha ujuzi unaohitajika na waajiri.

Naye Ofisa Mawasiliano wa  taasisi ya African Leadership Initiative for Impact, Yusra Abdulbastwa, alisema Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050,  inalenga kujenga uchumi wenye ushindani unaotegemea ubunifu, mabadiliko ya kidijitali, viwanda na ujasiriamali.

Alisema moja ya vipaumbele vya dira hiyo ni kuweka mazingira yatakayowawezesha vijana kuanzisha biashara, kupata fursa za uwekezaji na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.

“Serikali inataka vijana wasiishie kutafuta ajira pekee, bali pia wawe waajiri,” alisema.

Yusra  pia aliwahimiza wanafunzi kukumbatia matumizi ya akili unde  (AI), akieleza kuwa teknolojia hiyo haitachukua nafasi ya kila mtu, lakini wale watakaoshindwa kujifunza kuitumia wanaweza kupitwa na wenzao watakaoimudu.

Alisema stadi kama huruma, kufanya uamuzi wenye kuzingatia maadili, uongozi, maono na tabia njema zitaendelea kuwa muhimu kwa sababu ni vigumu kwa AI kuzifanikisha kikamilifu.

“Watu wanaojua kutumia AI watachukua nafasi ya wale wasioijua,” alisema.

Kwa upande wake, mhitimu wa kidato cha sita wa mwaka 2026, Buminganyikani Metson, alisema mkutano huo ulimfundisha umuhimu wa kujitokeza katika maeneo ambako fursa hutengenezwa.

Aliwahimiza vijana wenzake kuhudhuria semina, makongamano na matukio yanayowalenga vijana hata kama hayatoi malipo ya moja kwa moja.

“Huenda usilipwe kwa kuhudhuria tukio, lakini watu utakaokutana nao wanaweza kukufungulia milango ya fursa zinazoweza kubadilisha maisha yako,” alisema.

Kwa ujumla, washiriki wa mkutano huo walikubaliana kuwa mafanikio katika soko la ajira la sasa hayategemei tena vyeti vya kitaaluma pekee, bali yanahitaji pia ujuzi wa vitendo, mtandao mpana wa kitaaluma na uwezo wa kuendana na mabadiliko ya kasi ya uchumi na teknolojia.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

VIJANA NA MAMA LISHE WANUFAIKA MKOPO IRAMBA, SINGIDA ‎

Next

Hichilema ashinda tena urais Zambia

Recent Posts

  • Usaliti wa ACT – Wazalendo, Chadema katika sura pana
  • Serikali yaeleza kusuasua mradi wa Hospitali ya Singida – 3
  • FYATU MFYATUZI: Naunda tume tatu kuchunguza tume
  • Upinzani na safari ya ujenzi wa kizazi kipya chenye ushawishi
  • NIKWAMBIE MAMA: Mkulima na mfugaji ni gego na ufizi, havitengani

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme