Mourinho Amkingia Kifua Mbappe Kwenye Bio za Ballon d’Or

MADRID, Hispania: Kocha wa Real Madrid, Jose Mourinho, amesema mshambuliaji wa timu hiyo, Kylian Mbappe, ndiye anayestahili kushinda tuzo ya Ballon d’Or mwaka huu, akisisitiza kuwa tuzo hiyo inapaswa kutolewa kwa mchezaji bora zaidi duniani badala ya kuzingatia mafanikio ya timu katika Kombe la Dunia au Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Mourinho ametoa kauli hiyo Jumamosi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mchezo wa Real Madrid dhidi ya Malaga katika Ligi Kuu ya Hispania.

“Wachezaji bora duniani wapo wawili, watatu au wanne, na tunawajua. Wapo hapa,” amesema Mourinho.

Kocha huyo amesema kwa mtazamo wake, Mbappe ndiye anayestahili zaidi tuzo hiyo kutokana na mafanikio yake binafsi msimu huu, akirejea rekodi ya mshambuliaji huyo wa Ufaransa kuwa mfungaji bora wa muda wote katika historia ya Kombe la Dunia.

Mbappe ni miongoni mwa wagombea wa tuzo hiyo baada ya kumaliza msimu uliopita akiwa mfungaji bora wa La Liga, Ligi ya Mabingwa Ulaya pamoja na Kombe la Dunia 2026, licha ya kutwaa bila ubingwa mkubwa wa timu.

Wachezaji wengine wanaowania tuzo hiyo ni pamoja na mshambuliaji wa England, Harry Kane, kiungo wa Hispania na bingwa wa Kombe la Dunia, Rodri, pamoja na nyota wa Paris Saint-Germain, Ousmane Dembele na Khvicha Kvaratskhelia.

Mbappe aliendelea kuonyesha ubora wake baada ya kufunga mabao matatu katika ushindi wa Real Madrid wa 4-1 dhidi ya Real Sociedad Jumatano.

Akizungumzia vigezo vya Ballon d’Or, Mourinho amesema mafanikio ya timu pekee hayapaswi kuwa msingi wa kumpa mchezaji tuzo hiyo.

“Huwezi kumpa mchezaji Ballon d’Or kwa sababu tu ameshinda Ligi ya Mabingwa au Kombe la Dunia,” amesema.

Mourinho ametaja baadhi ya wachezaji waliowahi kushinda tuzo hiyo kama mifano ya wachezaji ambao walikuwa na kiwango cha kipekee binafsi, akiwemo Diego Maradona, Ronaldinho, Ronaldo Nazario, Cristiano Ronaldo, Lionel Messi na Zinedine Zidane.

Amesema endapo tuzo hiyo ingelenga zaidi mafanikio ya kushinda Ligi ya Mabingwa, basi ingepewa kocha wa Paris Saint-Germain, Luis Enrique, huku kwa upande wa timu ya taifa ya Hispania ikistahili kwenda kwa Luis de la Fuente.

Kwa mujibu wa Mourinho, Ballon d’Or inapaswa kumtambua mchezaji bora zaidi duniani kwa kiwango chake binafsi, na si tu mafanikio ya timu aliyochezea.