Video: Wabunge 324 Wamthibitisha Ndejembi kuwa Makamu wa Rais
Global Publishers
August 28, 2026
48 views
0 Comments
Wabunge 324 wamepiga kura za “Ndiyo” kumthibitisha Makamu wa Rais Mteule, Deogratius John Ndejembi, kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kura hiyo imefanyika leo, Agosti 28, 2026, katika kikao cha Bunge jijini Dodoma, kufuatia jina la Ndejembi kuwasilishwa kwa ajili ya uthibitisho.
Katika mchakato huo, hakukuwa na kura ya “Hapana” wala kura iliyoharibika, hivyo Ndejembi amepata uungwaji mkono wa asilimia 100 ya kura zilizopigwa.
Uthibitisho huo unafungua njia kwa Ndejembi kuapishwa rasmi na kuanza majukumu yake kama Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
