Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Serayah Aachana na Mchumba wake Joey, Afichua Madai ya Usaliti

By admin
August 26, 2026 1 Min Read
Comments Off on Serayah Aachana na Mchumba wake Joey, Afichua Madai ya Usaliti

Global Publishers
August 26, 2026
42 views
0 Comments

Muigizaji wa filamu na mwanamitindo Serayah ametangaza kuachana na mchumba wake, rapa Joey Bada$$, huku akidai kuwa msanii huyo alikuwa akimsaliti mara kwa mara katika kipindi cha uhusiano wao.

Serayah, anayefahamika pia kwa nafasi yake katika tamthilia Empire, amedai kuwa usaliti huo uliendelea kujitokeza katika vipindi mbalimbali vya uhusiano wao, ikiwemo wakati alipokuwa akipitia changamoto za maisha.

Wawili hao walikutana mwaka 2021 kupitia sherehe ya siku ya kuzaliwa ya rafiki yao na baadaye wakaanza uhusiano wa kimapenzi.

Uhusiano wao uliendelea kwa miaka kadhaa, ambapo mwaka 2025 walipata mtoto pamoja na kutangaza uchumba wao.

Hata hivyo, uhusiano huo umefikia mwisho huku Serayah akieleza madai ya kutoridhishwa na mwenendo wa Joey Bada$$ katika kipindi walichokuwa pamoja.

Taarifa kuhusu kuvunjika kwa uhusiano wao zimeibua hisia mbalimbali miongoni mwa mashabiki, hasa kutokana na wawili hao kuwa wamekuwa wakionekana pamoja hadharani na kushirikiana katika malezi ya mtoto wao.

Hadi sasa, Joey Bada$$ hajatoa maelezo ya kina kuhusu madai yaliyotolewa na Serayah.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo Agosti 26, 2026

Next

Karol G atoa Bilioni 3.1 Kusaidia Waathirika wa Tetemeko Colombia

Recent Posts

  • Dili la Sh Bilioni 418! Liverpool Yafikia Makubaliano na PSG kwa Barcola
  • Droo ya UEFA Champions League Msimu wa 2026/27 Kufanyika Leo Monaco
  • Kesi ya Uhaini ya Lissu Yaendelea leo;- Maswali Mazito Yaibuka Katika Dodoso la Serikali
  • Nafasi za Kazi Wezesha Mzawa Microfinance – Loan Officer, Mwisho wa Maombi Agosti 31, 2026
  • Safari Mpya Imeanza! Fahamu Mchezo wa 3 Fisher Cats Meridianbet

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme