Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Burudani

Harmonize Afichua Wasanii Walio kwenye Albamu Yake Mpya “31”

By admin
August 26, 2026 1 Min Read
Comments Off on Harmonize Afichua Wasanii Walio kwenye Albamu Yake Mpya “31”

Msanii wa Bongo Fleva, Harmonize, ameweka wazi orodha ya nyimbo zitakazopatikana katika albamu yake mpya inayokwenda kwa jina la “31”, ambayo inatarajiwa kutoka hivi karibuni.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Harmonize ameshirikisha mashabiki wake orodha ya nyimbo 14 zitakazounda albamu hiyo, huku akitangaza kuwa inatarajiwa rasmi kutoka Septemba 4, 2026.

Albamu hiyo imebeba ushirikiano mbalimbali kutoka kwa wasanii wakubwa ndani na nje ya Tanzania, akiwemo Marioo, Young Lunya, Jay Melody, Mayorkun, Darkoo, Yemi Alade, Rayvanny na Sofia Nzau, pamoja na wasanii wengine.

Kwa mujibu wa orodha hiyo, Harmonize anatarajiwa kuendelea kuonyesha uwezo wake wa kuunganisha muziki wa Bongo Fleva na ladha mbalimbali za kimataifa kupitia nyimbo zitakazopatikana kwenye albamu hiyo.

Harmonize, ambaye ni miongoni mwa wasanii waliofanikiwa kujenga jina kubwa katika muziki wa Tanzania, tayari ameachia albamu kadhaa zilizofanya vizuri, zikiwemo “Afro East” iliyotoka mwaka 2020, “High School” mwaka 2021 na “Made For Us” mwaka 2022.

Kwa sasa, Harmonize anaendelea kufanya vizuri kupitia wimbo wake “Beautiful”, ambao pia umejumuishwa katika albamu mpya ya “31”.

Albamu hiyo inatarajiwa kuwa miongoni mwa miradi mikubwa ya Harmonize kwa mwaka huu, huku mashabiki wakisubiri kwa hamu kuona namna atakavyowasilisha kazi hizo mpya pamoja na ushirikiano wa wasanii mbalimbali.

Stori na Na Didas Didas | GPL

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Airtel Fursa Lab Yazinduliwa Upya, Zaidi ya Watu 5,800 Wanufaika

Next

Kesi ya Uhaini: Lissu Akabiliana na Maswali ya Upande wa Jamhuri

Recent Posts

  • Kesi ya Uhaini ya Lissu Yaendelea leo;- Maswali Mazito Yaibuka Katika Dodoso la Serikali
  • Nafasi za Kazi Wezesha Mzawa Microfinance – Loan Officer, Mwisho wa Maombi Agosti 31, 2026
  • Safari Mpya Imeanza! Fahamu Mchezo wa 3 Fisher Cats Meridianbet
  • Europa League Kuamua! Salah Aongoza Trabzonspor Kwenye Mechi ya Marudiano
  • Watanzania 173 Warejea Nchini kwa Hiari Kutoka Afrika Kusini

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme