Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Michezo

Allen Robinson Astaafu NFL Baada ya Miaka 11, Aanza Maisha Mpya

By admin
August 26, 2026 1 Min Read
Comments Off on Allen Robinson Astaafu NFL Baada ya Miaka 11, Aanza Maisha Mpya

Global Publishers
August 26, 2026
12 views
0 Comments

Mchezaji wa zamani wa Ligi ya Soka ya Marekani (NFL), Allen Robinson, ametangaza kustaafu kucheza soka la Marekani akiwa na umri wa miaka 33, baada ya kutumia miaka 11 katika ligi hiyo.

Robinson alitangaza uamuzi huo Jumatatu, Agosti 24, kupitia ujumbe kwenye ukurasa wake wa Instagram, akiambatanisha video iliyosimulia safari yake ya kimichezo.

Robinson alianza kucheza NFL mwaka 2014 baada ya kuchaguliwa na Jacksonville Jaguars. Mwaka wake wa pili katika ligi ulikuwa wa kipekee kwake baada ya kuongoza ligi kwa kufunga touchdown 14 na kukusanya yadi 1,400, kiwango kilichomuwezesha kuchaguliwa katika Pro Bowl yake pekee.

Baada ya kuondoka Jacksonville Jaguars, Robinson aliwahi kuichezea Chicago Bears, Los Angeles Rams, Pittsburgh Steelers na Detroit Lions.

Mchezo wake wa mwisho katika NFL ulikuwa mwaka 2024 akiwa na Detroit Lions, huku akiwa hakushiriki msimu wa 2025.

Katika kipindi chake cha miaka 11 katika NFL, Robinson alimaliza akiwa na jumla ya receptions 565, receiving yards 7,058 na touchdown 43.

Robinson amesema sasa anaanza sura mpya ya maisha yake, huku akieleza shukrani kwa safari yake ya soka, pamoja na watu mbalimbali aliokutana nao na waliomsaidia katika kipindi chote cha maisha yake ya kimichezo.

Uamuzi huo unahitimisha safari ya miaka 11 ya Robinson katika NFL, ambapo aliibuka miongoni mwa wapokeaji muhimu wa pasi katika baadhi ya misimu ya ligi hiyo.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

TAKRIBANI WATOTO 14 WAMETEKETEA WAKIWA HOSPITALINI, NCHINI PAKISTAN

Next

Tundu Lissu Amaliza Kujitetea, Mahakama Yapumzika kabla ya Dodoso

Recent Posts

  • UN YAITAKA TANZANIA KUSITISHA UHAMISHAJI WA WAMASAI NGORONGORO NA LOLIONDO
  • ‘NCHIMBI SIO CHAWA’ – WARIOBA
  • TUME YA ULINZI WA TAARIFA BINAFSI YAANZA UKAGUZI KWA WAKUSANYAJI NA WACHAKATAJI WA TAARIFA HIZO NCHINI.
  • HALMASHAURI YA MAFINGA MJINI HATUJAFUKUZA WATUMISHI WA AFYA BADO TUNAUHITAJI -KAIMU MKURUGENZI
  • SERIKALI KUTUMIA SH1.39 TRILIONI KUKARABATI VIFAA TIBA

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme