Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Michezo

Jamal Bakhresa Afungiwa Kujihusisha na Mpira kwa Mwaka Mmoja

By admin
August 23, 2026 1 Min Read
Comments Off on Jamal Bakhresa Afungiwa Kujihusisha na Mpira kwa Mwaka Mmoja

Global Publishers
August 23, 2026
1,050 views
0 Comments

Kiongozi wa Azam FC, Jamal Bakhresa, amefungiwa kujihusisha na shughuli za mpira wa miguu kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Agosti 22, 2026, adhabu hiyo inahusishwa na vitendo vya utovu wa nidhamu vinavyodaiwa kufanywa na Bakhresa kabla na baada ya mchezo wa fainali ya Kombe la CRDB uliochezwa kisiwani Pemba.

Bakhresa alifikishwa mbele ya Kamati ya Nidhamu ya TFF kujibu tuhuma mbalimbali za ukiukwaji wa kanuni za nidhamu. Katika mchakato wa kusikilizwa kwa shauri hilo, alisaidiwa na Wakili Alex Mushumbusi.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Bakhresa alikiri baadhi ya makosa yaliyowasilishwa mbele ya kamati hiyo.

Mbali na adhabu ya kufungiwa kujihusisha na shughuli za mpira kwa mwaka mmoja, Bakhresa pia ameamriwa kulipa faini kutokana na makosa yaliyobainishwa. Aidha, ameahidi kutorudia vitendo hivyo.

Kamati ya Nidhamu ya TFF imesema uamuzi huo umetolewa kwa kuzingatia Ibara ya 11(f) ya Kanuni za Nidhamu za TFF, Toleo la mwaka 2021.

Adhabu hiyo inamaanisha Bakhresa hataruhusiwa kushiriki katika shughuli za mpira wa miguu kwa kipindi kilichowekwa na kamati, huku uamuzi huo ukilenga kuimarisha nidhamu na kuzingatiwa kwa kanuni katika soka la Tanzania.

Stori na Florah Anderson | GPL – TUDACO

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Meghan Markle Aanza Ukurasa Mpya wa Uigizaji Baada ya Kuondoka Suits

Next

WAZIRI MKUU AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA MWANANYAMALA

Recent Posts

  • Rais Samia Ateua na Kuhamisha Wakuu Wa Mikoa, Makatibu Tawala
  • RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI NA UHAMISHO WA WAKUU WA MIKOA
  • Mavunde Ampongeza Ndejembi “Ni Kiongozi Kijana, Mwadilifu na Mzalendo” – Video
  • MWABUKUSI: KUFUKUZWA CCM KWA NCHIMBI HAKUMVUI MOJA KWA MOJA UMAKAMU WA RAIS
  • Dili la Sh Bilioni 418! Liverpool Yafikia Makubaliano na PSG kwa Barcola

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme