Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Burudani

Ariana Grande Amkosoa Trump, Akataa Muziki Wake Kutumika Kisiasa

By admin
August 23, 2026 2 Min Read
Comments Off on Ariana Grande Amkosoa Trump, Akataa Muziki Wake Kutumika Kisiasa

Msanii maarufu wa Marekani, Ariana Grande, amemkosoa vikali Rais Donald Trump na timu yake baada ya kutumia wimbo wake “We Can’t Be Friends (Wait for Your Love)” katika video ya TikTok iliyokuwa ikiunga mkono sera za Trump kuhusu watu waliobadili jinsia.

Video hiyo iliyowekwa na akaunti rasmi ya Team Trump Alhamisi, Agosti 20, 2026, ilimuonyesha Trump akielekea kwenye jukwaa la mkutano huku wimbo huo wa Grande ukitumika kama sauti ya video.

Katika video hiyo pia kulikuwa na ujumbe unaosema kuwa wanaume hawawezi kupata watoto na hawapaswi kushindana katika michezo ya wanawake.

Grande, ambaye amekuwa akipinga matumizi ya muziki wake katika kampeni za kisiasa za Trump, alijibu kwenye maoni ya video hiyo akimtaka timu ya Trump kuacha kutumia kazi zake.

“Never use my music again. Also, your truth is false,” aliandika Grande, akimaanisha kuwa muziki wake usitumike tena na pia kupinga ujumbe uliokuwa kwenye video hiyo.

Maoni yake hata hivyo baadaye hayakuonekana tena kwenye chapisho hilo.

Hii si mara ya kwanza kwa Grande kukosoa matumizi ya muziki wake na utawala wa Trump. Juni mwaka huu, White House ilitumia wimbo wake “Bye” katika video iliyohusisha operesheni za Immigration and Customs Enforcement (ICE).

Grande ni miongoni mwa wasanii kadhaa wakubwa ambao wamewahi kupinga matumizi ya nyimbo zao na kampeni au shughuli zinazohusishwa na Trump, wakiwemo Sabrina Carpenter, Katy Perry, SZA, Adele, Rihanna, Céline Dion, Elton John, Neil Young na wengine.

Hatua hiyo inaendelea kuonyesha mvutano kati ya wasanii mbalimbali na timu ya Trump kuhusu matumizi ya muziki wao katika maudhui ya kisiasa bila ridhaa yao.https://www.youtube.com/watch?v=c2osqc-bV1E

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

NDOA YA MZEE CHRISTOPHER MWANGOSI NA CHRISTINA YATIKISA MBEYA

Next

Ajira NIT 2026: Nafasi 23 Zatangazwa, Mwisho wa Maombi Agosti 28, 2026

Recent Posts

  • Kesi ya Uhaini ya Lissu Yaendelea leo;- Maswali Mazito Yaibuka Katika Dodoso la Serikali
  • Nafasi za Kazi Wezesha Mzawa Microfinance – Loan Officer, Mwisho wa Maombi Agosti 31, 2026
  • Safari Mpya Imeanza! Fahamu Mchezo wa 3 Fisher Cats Meridianbet
  • Europa League Kuamua! Salah Aongoza Trabzonspor Kwenye Mechi ya Marudiano
  • Watanzania 173 Warejea Nchini kwa Hiari Kutoka Afrika Kusini

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme