Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Mradi wa Julius Nyerere Watikisa Sekta ya Nishati kwa MW 2,115

By admin
August 22, 2026 2 Min Read
Comments Off on Mradi wa Julius Nyerere Watikisa Sekta ya Nishati kwa MW 2,115

Global Publishers
August 22, 2026
78 views
0 Comments

Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) umeingia katika hatua muhimu katika historia ya sekta ya nishati nchini Tanzania, baada ya kufikia uwezo wa kuzalisha megawati 2,115 za umeme.

Mradi huo uliopo Rufiji, Mkoa wa Pwani, unatarajiwa kuzinduliwa rasmi kesho, Agosti 22, 2026, katika hafla itakayowakutanisha viongozi pamoja na wadau mbalimbali.

JNHPP umegharimu takribani Shilingi trilioni 7.452, huku ukielezwa kuwa miongoni mwa miradi mikubwa zaidi ya uzalishaji umeme kutekelezwa nchini kwa kutumia fedha za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Wizara ya Nishati, mradi huo tayari umeanza kutoa mchango mkubwa katika Gridi ya Taifa. Katika kipindi kilichoishia Mei 31, 2026, JNHPP ulichangia takribani asilimia 44.9 ya umeme wote uliozalishwa na kuingizwa kwenye gridi.

Uwezo huo unatarajiwa kusaidia kukidhi ongezeko la mahitaji ya umeme nchini, ambayo yalifikia kiwango cha juu cha takribani MW 2,199.06 Februari 4, 2026.

Mradi wa Julius Nyerere unatarajiwa kuwa na nafasi kubwa katika kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini, pamoja na kusaidia shughuli za uzalishaji, biashara na ukuaji wa uchumi.

Uzinduzi rasmi wa mradi huo kesho unatajwa kuwa hatua muhimu katika historia ya sekta ya nishati Tanzania, huku Serikali ikiendelea kuweka mkazo katika kuongeza uzalishaji wa umeme na kuimarisha uwezo wa Gridi ya Taifa.

Stori na Anifa Mwegelo | GPL – TUDACO

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Dogo Janja Afunguka Kuhusu Ndoa yake na Irene Uwoya – Video

Next

Kairuki apongeza upanuzi huduma za intaneti – HabariLeo

Recent Posts

  • MWABUKUSI: KUFUKUZWA CCM KWA NCHIMBI HAKUMVUI MOJA KWA MOJA UMAKAMU WA RAIS
  • Dili la Sh Bilioni 418! Liverpool Yafikia Makubaliano na PSG kwa Barcola
  • Droo ya UEFA Champions League Msimu wa 2026/27 Kufanyika Leo Monaco
  • Kesi ya Uhaini ya Lissu Yaendelea leo;- Maswali Mazito Yaibuka Katika Dodoso la Serikali
  • Nafasi za Kazi Wezesha Mzawa Microfinance – Loan Officer, Mwisho wa Maombi Agosti 31, 2026

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme