Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Aliyembaka mtoto wa mwaka mmoja akwama rufaa, ahukumiwa jela maisha

By admin
August 19, 2026 3 Min Read
Comments Off on Aliyembaka mtoto wa mwaka mmoja akwama rufaa, ahukumiwa jela maisha

Arusha. Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Tanga, imetupilia mbali rufaa ya Greyson Msemo aliyekuwa akipinga hukumu ya kifungo cha miaka 30 jela baada ya kukutwa na hatia ya kumbaka mtoto wa mwaka mmoja na miezi minne na badala yake imeongeza adhabu hiyo kuwa kifungo cha maisha.

Greyson alishtakiwa mahakama ya Wilaya Pangani kwa kosa la ubakaji kinyume na kifungu cha 130(1) (2) (e) na 131 (1) cha Kanuni ya Adhabu, kosa alilodaiwa kulitenda Septemba Mosi, 2025 katika eneo la Funguni,Wilaya ya Pangani Mkoa wa Tanga.

Uamuzi uliobatilisha adhabu hiyo na kumuongezea kuwa kifungo cha maisha jela umetolewa na Jaji Happiness Ndesamburo, Agosti 18,2026.



Jaji Ndesamburo amesema baada ya kupitia kwa makini hoja za pande zote na kumbukumbu nzima ya kesi, ameridhika kuwa upande wa mashtaka ulithibitisha shtaka dhidi ya Greyson bila kuacha shaka yoyote.

Jaji amesema ingawa mtoto aliyedaiwa kufanyiwa ukatili huo hakutoa ushahidi mahakamani kutokana na umri wake wa mwaka mmoja na miezi minne, hali hiyo haikufanya kesi ya upande wa mashtaka kuwa na dosari.

Katika kuthibitisha kesi hiyo upande wa mashtaka ulikuwa na mashahidi wanne ambapo shahidi wa kwanza alikuwa bibi wa mtoto huyo na siku ya tukio akiwa anasuka mitende, alimtuma mjukuu wake mwingine kumletea Msemo maji ya kunywa.

Alidai mtoto huyo aliporudi, naye alitoka nje na kumkuta Msemo akiwa amemshikilia mwathirika wa tukio hilo mapajani huku akifanya kitendo hicho cha kikatili kwa mtoto huyo.

Alidai alipopiga kelele, Msemo alivuta suruali yake, ambapo alimwita mumewe na  baada ya watu kukusanyika eneo hilo Msemo alikamatwa na kupelekwa Kituo cha Polisi Pangani.

Shahidi wa nne ambaye ni mama wa mwathirika wa tukio hilo, alisema kuwa alimwacha mtoto wake chini ya uangalizi wa mama yake na kwenda msibani Muheza ambapo alipopata taarifa kuhusu tukio hilo na kurudi, alikuta mtoto tayari amefikishwa hospitalini kwa matibabu.

Kwa upande wa utetezi, Msemo alikana kutenda kosa hilo na kudai hakuwajua watu waliohusika katika jambo hilo na kuwa ushahidi wa upande wa mashtaka haukuwa wa kweli.

Akiwa hajaridhishwa na uamuzi huo alikata rufaa akiwa na sababu tano ikiwemo hakimu alikosea kisheria kwa kumtia hatiani bila ushahidi kutoka kwa mwathirika wa tukio hilo, ushahidi wa mashtaka ulikuwa dhaifu na wenye shaka.

Sababu nyingine alidai kuwa Hakimu alikosea kwa kushindwa kubaini kuwa mrufani (mshtakiwa kwa wakati huo) hakuwa mzima wa akili na kuwa kesi dhidi yake haikuthibitishwa bila kuacha shaka yoyote.

Jaji Ndesamburo amesema sheria inatambua mazingira ambayo kosa linaweza kuthibitishwa bila mwathirika kutoa ushahidi, ikiwamo pale mwathirika akiwa na umri mdogo sana.

Kuhusu ushahidi wa tukio, Jaji amesema ushahidi wa bibi wa mtoto ulikuwa wa moja kwa moja na wa kuaminika, kwani alimkuta Msemo katika eneo la tukio na baadaye alipiga kelele , huku ushahidi huo ukiungwa mkono na ushahidi wa kitabibu.

Jaji amesema matokeo ya uchunguzi wa kitabibu yalionyesha kuwepo kwa majeraha katika sehemu za siri za mtoto na kuwa ni sheria iliyoidhinishwa kwamba hata kupenya kidogo kunatosha kuhalalisha kosa hilo la ubakaji.

Jaji pia alikataa hoja ya Msemo kwamba upande wa mashtaka ulipaswa kuwaita majirani, kiongozi wa kijiji, Ofisa Mtendaji wa Kijiji na askari aliyetoa PF3.

Amesema watu hao hawakuwa mashahidi muhimu kwa kuwa hakuna ushahidi ulioonyesha kuwa walishuhudia tukio hilo au ushahidi wao ungeongeza ukweli ambao haukuwa umeelezwa na mashahidi waliotoa ushahidi.

Kuhusu madai ya Msemo kwamba hakuwa mzima wa akili, Jaji amesema hakuna jambo hilo katika kumbukumbu za kesi lililoonyesha kuwa alikuwa na tatizo hilo na  hakukuwa na tabia isiyo ya kawaida iliyorekodiwa wakati wa kesi, hakutoa utetezi wa kichaa na alitoa utetezi wake, hivyo madai hayo hayakuwa na msingi.

Jaji amesema baada ya kutathmini upya ushahidi, Mahakama iliridhika kuwa vipengele muhimu vya kosa, ambavyo ni umri wa mwathiriwa, kupenya na utambulisho wa mshtakiwa vilithibitishwa bila shaka yoyote.

Hata hivyo, Jaji alibaini kuwa Mahakama ya Wilaya ya Pangani ilikosea katika kutoa adhabu ya kifungo cha miaka 30 badala ya kifungo cha maisha na kuwa mtoto alikuwa na umri wa mwaka mmoja na miezi minne, alikuwa chini ya miaka 10, hivyo kifungu cha 131(3) cha Kanuni ya Adhabu kinataka adhabu ya kifungo cha maisha.

“Kwa kuwa sikuona msingi wowote wa rufaa, rufaa hiyo imetupiliwa mbali kabisa. Ninarekebisha hukumu hiyo kwa kubadilisha kifungo cha miaka 30 na kuwa kifungo cha maisha jela ,” amehitimisha Jaji Ndesamburo.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

JWTZ kutoa matibabu bure | Mwananchi

Next

Kibaha yaimarisha upimaji ardhi kupunguza migogoro

Recent Posts

  • Saratani ya mlango wa kizazi yaongoza kwa vifo Tanzania
  • Makandarasi, kampuni za ujenzi walalamikia faini TRA
  • Waziri wa zamani wa Ukraine ataka uchaguzi vitani
  • Tanzania yaikabidhi DRC vifaa tiba vya Sh220 milioni kukabili Ebola
  • Mjane aporwa ardhi kwa madai hakuzaa na mumewe, RC aingilia kati

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme