*WAKULIMA WA KITOMONDO WANUFAIKA NA HUDUMA YA MAWASILIANO*
Wakulima katika Kijiji cha Kitomondo wamenufaika na kuimarika kwa huduma za mawasiliano ambayo imeondoa changamoto kubwa ya ugawaji dawa, pembejeo na upatikanaji wa masoko kupitia mfumo wa kidijitali.
Akizungumzia mafanikio hayo, Katibu wa Chama cha Ushirika – Kitomondo (AMCOS) Yusuf Mansouri amesema hapo awali walikuwa wanapata changamoto kubwa kwa wakulima kuchelewa kupata huduma lakini baada ya Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kuwawezesha mnara wa mawasiliana changamoto hizo zimemalizika.
Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) imetekeleza mradi wa ujenzi wa Minara 768 ya kimkakati ya mawasiliano wenye lengo la kuwezesha upatikanaji wa huduma ya mawasiliano kwa wananchi waishio yasiyo maeneo machache ya mjini na vijijini yenye yasiyo na mvuto wa kibiashara kwa watoa huduma.




