Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Burudani

Dk Nchimbi Atangaza Kujiuzulu Umakamu wa Rais na Kustaafu Siasa

By admin
August 25, 2026 2 Min Read
Comments Off on Dk Nchimbi Atangaza Kujiuzulu Umakamu wa Rais na Kustaafu Siasa

Global Publishers
August 25, 2026
828 views
0 Comments

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Emmanuel John Nchimbi, ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo na kustaafu siasa pamoja na utumishi wa umma.

Dk Nchimbi ametoa taarifa hiyo leo Jumanne, Agosti 25, 2026, akisema amemwandikia Rais Samia Suluhu Hassan barua ya kumjulisha kuhusu uamuzi wake wa kujiuzulu nafasi ya Makamu wa Rais, kuanzia Septemba 4, 2026.

Katika taarifa yake, Dk Nchimbi amesema uamuzi huo umetokana na ahadi aliyompa Rais Samia wakati alipoteuliwa kushika nafasi hiyo, kwamba angeendelea kumsaidia katika majukumu yake kwa uaminifu na uwezo wake wote, na angeachia nafasi hiyo iwapo angehisi Rais anahitaji mabadiliko.

“Nimejiridhisha pasipo shaka kuwa Mhe. Rais anatamani mabadiliko, hivyo nimeamua kutimiza ahadi yangu,” amesema Dk Nchimbi katika taarifa yake.

Aidha, amemshukuru Rais Samia pamoja na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa imani waliyoonyesha kwake, huku akiwashukuru Watanzania kwa ushirikiano na kumuunga mkono katika kipindi chake cha utumishi.

Dk Nchimbi amesisitiza kuwa licha ya kustaafu siasa na utumishi wa umma, ataendelea kuwa raia mwema na kulitumikia taifa katika nafasi nyingine.

Kujiuzulu kwake kunakuja ikiwa ni takribani mwaka mmoja tangu alipoanza kushika nafasi ya Makamu wa Rais, na endapo uamuzi huo utaidhinishwa, hatua hiyo itakuwa miongoni mwa matukio ya kipekee katika historia ya uongozi wa Tanzania.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Video: Simanzi Kihesa, Mrembo wa Miaka 23 Afariki Ndani ya Chumba Chake

Next

Rais Samia Awatakia Waislamu Kheri katika Maadhimisho ya Maulid

Recent Posts

  • UN YAITAKA TANZANIA KUSITISHA UHAMISHAJI WA WAMASAI NGORONGORO NA LOLIONDO
  • ‘NCHIMBI SIO CHAWA’ – WARIOBA
  • TUME YA ULINZI WA TAARIFA BINAFSI YAANZA UKAGUZI KWA WAKUSANYAJI NA WACHAKATAJI WA TAARIFA HIZO NCHINI.
  • HALMASHAURI YA MAFINGA MJINI HATUJAFUKUZA WATUMISHI WA AFYA BADO TUNAUHITAJI -KAIMU MKURUGENZI
  • SERIKALI KUTUMIA SH1.39 TRILIONI KUKARABATI VIFAA TIBA

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme