Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Stamico yawekeza Sh milioni 40 mkaa mbadala Geita – HabariLeo

By admin
August 26, 2026 2 Min Read
Comments Off on Stamico yawekeza Sh milioni 40 mkaa mbadala Geita – HabariLeo

GEITA: SHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limetoa ufadhili wa jumla ya Sh milioni 40 kwa wazalishaji wa mkaa mbadala mkoani Geita ambao ni Taasisi ya Wanawake na Samia ili kuongeza matumizi ya nishati safi nchini.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Samia mkoani Geita, Adelina Kabakama ametoa taarifa hiyo mbele ya viongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa kwa Mwaka 2026.

Kabakama amesema kupitia mradi huo Taasisi ya Wanawake na Samia Geita itashirikiana na STAMICO kuunga mkono jitihada za kuzalisha na kuuza mkaa wa nishati safi.

Amesema hatua hiyo inalenga kutekeleza mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati safi ya kupikia kwa mwaka 2024/34 kwa kuhakikisha asilimia 80 ya watanzania wanatumia Nishati safi ifikapo 2034.

“Mradi huu unanufaisha wananchi kwani gharama za mkaa huu ni nafuu, pia mkaa huu ni nishati rafiki kwa mazingira kwani hupunguza matumizi ya kuni na kupunguza ukataji wa miti ili kutengeneza mikaa.

“Kwa sasa tunasambaza wastani wa tani 03 kwa mwezi, na tumenuwia kupeleka kwenye taasisi mbalimbali za umma na kulingana na ongezeko la mahitaji”, amesema Kabakama.

Amesema ili kukidhi mahitaji, STAMICO imepanga kujenga kiwanda cha mkaa mbadala mkoani Geita ili kusogeza huduma kwa wateja na kuendelea kuweka ukaribu kwa watanzania kupata nishati safi kwa ukaribu”, amesema.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa kwa Mwaka 2026, Wazo Michael Mwang’oda amesema matumizi ya nishati safi ya kupikia inapaswa kuungwa mkono na kila mtu kwani inalenga kuimarisha usalama wa afya za binadamu na mazingira.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

OUT na Mzumbe Watangaza Nafasi 6 za Kazi, Mwisho wa Maombi Agosti 31

Next

Aishi na Uvimbe Miaka 20 Aomba Msaada wa Matibabu, Afunguka Mazito -Video

Recent Posts

  • RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI NA UHAMISHO WA WAKUU WA MIKOA
  • Mavunde Ampongeza Ndejembi “Ni Kiongozi Kijana, Mwadilifu na Mzalendo” – Video
  • MWABUKUSI: KUFUKUZWA CCM KWA NCHIMBI HAKUMVUI MOJA KWA MOJA UMAKAMU WA RAIS
  • Dili la Sh Bilioni 418! Liverpool Yafikia Makubaliano na PSG kwa Barcola
  • Droo ya UEFA Champions League Msimu wa 2026/27 Kufanyika Leo Monaco

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme