Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

ATOLEWA JIWE LA KILO 3.1 KWENYE KIBOFU

By admin
August 19, 2026 1 Min Read
Comments Off on ATOLEWA JIWE LA KILO 3.1 KWENYE KIBOFU

NA MWANDISHI WETU

 Madaktari Nchini Sri Lanka wamefanya upasuaji wa kuliondoa jiwe lenye uzito wa kilo 3.1 kwenye kibofu cha mkojo cha Mwanaume mwenye umri wa miaka 55.

Upasuaji huo umefanyika katika Hospitali Kuu ya Trincomalee, Mashariki mwa Sri Lanka, baada ya Mwanaume huyo kulazwa hospitalini kufuatia kupata kiharusi ambapo Madaktari waligundua tatizo hilo baada ya kubaini kuwa alikuwa akipata changamoto wakati wa kukojoa.

Jiwe hilo lilikuwa na urefu wa takribani sentimita 17, likiwa na ukubwa unaokaribiana na yai la mbuni na uzito unaokaribiana na wa Mtoto anayezaliwa, ambapo Daktari aliyeongoza upasuaji huo, Dkt. Prahalahan Balakrishnan amesema kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo, huenda likawa miongoni mwa mawe makubwa zaidi ya kibofu kuwahi kurekodiwa na kuondolewa kwa upasuaji.

Madaktari wanaamini jiwe hilo lilikuwa limejikusanya kwenye kibofu cha mgonjwa huyo kwa kipindi cha kati ya miaka mitano hadi 10, kwa sasa anaendelea kupata matibabu hospitalini kutokana na matatizo mengine ya kiafya, huku madaktari wakisema hali yake ni nzuri.

Hata hivyo, kwa mujibu wa Guinness World Records, rekodi ya jiwe kubwa la kibofu lililoondolewa ilikuwa ya jiwe lenye uzito wa kilo 1.9 na urefu wa sentimita 17.9, lililoondolewa Nchini Brazil mwaka 2003 huku jiwe lililoondolewa Sri Lanka likiwa na uzito mkubwa zaidi wa kilo 3.1.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

SERIKALI KUONGEZA NGUVU MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

Next

Ebola yazidi kutikisa DR Congo, vifo vyafikia 2,378

Recent Posts

  • Kilomita sita kufuata matibabu zawasukuma Kola kujenga zahanati 
  • FIFA IMEJIHARIBIA YENYEWE KWA MPANGO WA KOMBE LA DUNIA – MKUU WA LIGI KUU YA UINGEREZA
  • SERIKALI YATOA MIEZI SITA KUSAJILI MIUNDOMBINU MUHIMU YA TEHAMA
  • MAONESHO YA YST YAIBUA HAMASA YA SAYANSI KWA WANAFUNZI LINDI
  • Ebola yazidi kutikisa DR Congo, vifo vyafikia 2,378

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme