Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Subscribe
Close

Search

Habari

DCEA yateketeza ekari 603 za bangi Morogoro

By admin
August 17, 2026 2 Min Read
0

Dar es Salaam. Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeanza operesheni maalumu ya kuharibu mashamba ya bangi mkoani Morogoro, baada ya kubaini wakulima kuhamia maeneo ya mbali ndani na nje ya Hifadhi ya Mikumi.

Katika operesheni maalumu iliyofanyika kwa siku 14 katika vijiji vya Visengele na Lugenge wilayani Mvomero, DCEA imeteketeza ekari 603 za bangi,   kukamata magunia 49 ya bangi na watuhumiwa 13 kwa tuhuma za kujihusisha na kilimo cha dawa hizo za kulevya.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Jumatatu Agosti 17, 2026 Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo operesheni hiyo ni mwendelezo wa kampeni maalumu ya kudhibiti dawa za kulevya zinazozalishwa nchini, hususani bangi, huku akieleza kuwa mamlaka imebaini baadhi ya wakulima wamehamia maeneo ambayo hayajawahi kufikiwa na operesheni za awali.



Amesema pamoja na operesheni kufanyika katika maeneo hayo tangu mwaka 2023, bado wananchi wameendelea kulima bangi ndani ya Hifadhi ya Mikumi na maeneo ya nje ya hifadhi.

“Katika operesheni tulizozifanya safari hii tumegundua kwamba wamelima mbali zaidi ya maeneo ambayo operesheni zilishafanyika awali, wakidhani mamlaka itashindwa kufika katika maeneo hayo,” amesema Lyimo.

Lyimo amesema ukubwa wa mashamba yaliyobainika unaonyesha kuwa kilimo cha bangi bado ni changamoto katika baadhi ya maeneo ya Morogoro, hasa ndani ya hifadhi na katika vijiji vinavyozunguka maeneo ya mapori.

“Maeneo haya yako mbali sana na vijiji na makazi ya wananchi, lakini mamlaka itaweka intelijensia ya kutosha ili kuhakikisha kwamba hizi operesheni na hawa wahalifu tutaendelea kuwakamata,” amesema.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Masaji si tiba ya kila maumivu, wataalamu waonya

Next

Aliyedai fidia ya Sh40 milioni kwa kulea mimba ya mtoto asiye wake, agonga mwamba kortini

No Comment! Be the first one.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recent Posts

  • MAGAZETINI LEO IJUMAA AGOSTI 14/2026:TRA KUVUKA MALENGO KWAMGUSA BALOZI OMARI,MADAKTARI BINGWA WAPIGA KAMBI HOSPITAL YA TOSAMAGANGA IRINGA…
  • SUA YASISITIZA MAWASILIANO YA KISAYANSI KUFIKISHA MATOKEO YA UTAFITI KWA JAMII
  • MAHAFALI YA DARASA LA SABA 2026 ST DOMINIC SAVIO IRINGA PICHA ZOTE HIZI HAPA
  • ASKOFU MIHALI AWATAKA WAZAZI KUENDANA NA DIRA 2050 KWA KUWEKEZA KATIKA ELIMU
  • Ziara ya Rais Tshisekedi kufungua ukurasa mpya wa biashara, amani

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme